Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRNA), Dkt. Hussein Jaberi Ansari, amesema kuwa urithi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kujenga uhuru na uwezo wa taifa ni wa kipekee na unastahili kujivunia.
Akizungumza katika kipindi maalumu cha televisheni cha IRNA kilichopewa jina "Sayyid wa Iran Shahidi", Jaberi Ansari amesema kuwa ushahidi wa mafanikio hayo unaonekana wazi kupitia matukio na uzoefu wa hivi karibuni ambao Iran imeupitia.
Ameeleza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilijengwa juu ya msingi wa historia ndefu ya taifa la Iran, ustaarabu wake na mchango wa wasomi wake, huku akisisitiza kuwa uongozi wa Imam Ruhullah Khomeini (r.a.), mwanzilishi wa Jamhuri ya Kiislamu, na kuendelezwa kwa njia hiyo kwa takribani miongo minne chini ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, umeimarisha uhuru wa taifa, kulinda umoja wa ardhi ya Iran na kufufua uwezo wa kitaifa, jambo ambalo limechangia kufikiwa kwa mafanikio makubwa ya nchi hiyo.
Your Comment